Sinopsis
Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.
Episodios
-
Robert Francis Prevost achaguliwa kumrithi Papa Francis na kuchukua jina la Papa Leo XIV
22/05/2025 Duración: 20minMakala haya yanaangazia taarifa mbalimbali ikiwemo, Mmarekani Robert Francis Prevost, achaguliwa kuongoza kanisa katoliki duniani, akichukua jina la Papa Leo wa kumi na nne. Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chadema, chatumbukia katika sintofahamu zaidi kufuatia baadhi ya waliokuwa wajumbe wa kamati kuu ya chama, kutangaza kujiondoa kwenye chama hicho. Tarifa zingine utakazoskia, silaha za China zilizoagizwa na taifa la Falme za Kiarabu zimepatikana zikitumika na wapiganaji wa RSF nchini Sudan, na nchi jirani za India na Pakistan zashambiliana kwa silaha nzito na kuzua wasiwasi mkubwa katika maeneo ya mipakani.
-
Kuuawa kwa mbunge jijini Nairobi Kenya, Marekani kuzipatanisha Rwanda na DRC
03/05/2025 Duración: 20minMakala hii imeamgazia kuuawa kwa mbunge wa Kasipul Charles Ong'ondo Were, kwa kupigwa risasi na watu waliokuwa kwa pikipiki katika barabara ya Ngong Jijini Nairobi, jumatano, kukamatwa kwa mlinzi wake kiongozi wa chama cha upinzani cha NUP nchini Uganda, nao wawakilishi wa DRC na Rwanda wanaokutana Washington Marekani kusaini mkataba kuelekea makubaliano ya amani ya mashariki mwa DRC, siasa za Tanzania na kushambuliwa kwa kasisi wa kikatoliki na matukio kadhaa ya juma hili kutokea duniani
-
Mazishi ya papa Francis huko vatican, DRC na Rwanda zakubaliana kuelekea amani
26/04/2025 Duración: 20minMakala ya yaliyojiri wiki hii imeangazia mazishi ya kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, DRC na Rwanda zatia saini makubaliano kuhusu njia ya kupatikana amani ya mashariki mwa Congo, siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi wa oktoba, ziara ya rais wa Kenya William Ruto huko China, hali ya vita ya Sudan, vita ya Ukraine na huko Gaza Israeli, ni miongoni mwa Habari kuu za dunia zilizojiri kwa juma hili.
-
Vita ya Sudan kuingia mwaka wa tatu, Joseph Kabila arejea nchini DRC
19/04/2025 Duración: 20minVita ya sudan Kuingia katika mwaka wa tatu wiki hii, Kenya yatangaza marufuku ya biashara ya figo baada ya ufichuzi, rais wa zamani wa DRC arejea nchini aliwasili mjini Goma huku Marekani ikiitaka nchi ya Rwanda kuondoa wanajeshi wake mashariki mwa nchi hiyo, tumeangazia siasa za Tanzania kuelekea uchaguzi wa Oktoba, kule Sahel na wito wa rais wa Ghana wiki hii akiwataka viongozi wa nchi hizo kuungana pamoja na pia mkutano wa Paris kuhusu hatima ya vita ya Ukraine