Sinopsis
Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.
Episodios
-
Kizza Besigye wa Uganda ashtakiwa kwa uhaini, Kenya na Sudan zatofautiana kuhusu RSF
23/02/2025 Duración: 19minHabari za wiki hii ni pamoja na hali kule nchini Mashariki mwa DRC, utata wa kidplomasia uanozingira Kenya na Sudan, tutaangazia pia kesi ya kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye, lakini tutaangalia kipindi cha mpito nchini Niger. Tumedadisi pia hali kufikia sasa ya vita vya kule Gaza na misimamo ya viongozi mbalimbali wa ulimwengu.
-
Mkutano wa AU kuhusu mzozo wa DRC, waasi wa M23 waudhibiti mji wa Bukavu
15/02/2025 Duración: 20minMakala hii imeangazia mkutano wa viongozi wa Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia ambapo wamemchagua kiongozi wa tume ya Umoja wa Afrika AU kati ya wagombea watatu, lakini pia mapigano yanayoendelea kati ya waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda dhidi ya jeshi la serikali FARDC na ambao sasa wameudhibiti mji wa Bukavu huko Kivu kusini mashariki mwa DRC, mapigano ya nchini Sudan, siasa za Uganda na pia kwenye nchi za Afrika Magharibi. Lakini pia zoezi la ubadirishanaji wa mateka huko Gaza
-
Mkutano wa pamoja kati ya SADC na EAC kuhusu DRC
08/02/2025 Duración: 20minKwa sehemu kubwa makala ya mtazamo wako imeangazia kuhusu hali ya mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na mkutano wa pamoja kati ya jumuia ya Afrika mashariki EAC na jumuia ya Nchi za kusini mwa Afrika SADC kutafuta suluhu ya kudumu ya mzozo wa mashariki mwa DRC, huko Gabon upinzani umemtaka kiongozi wa mpito kuweka wazi msimamo wake kuhusu ushiriki wake katika uchaguzi mkuu, na hatua ya rais wa Marekani Donald Trump kukata ufadhili kwa shirika la misaada USAID pia Marekani kudhibiti eneo la Gaza
-
Juhudi za kimataifa katika kusaka amani ya mashariki mwa DRC
01/02/2025 Duración: 20minMakala ya yaliyojiri wiki hii kwa sehemu kubwa imejikita katika kudadavua hali yausalama wa mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ambako tangu mwanzo wa juma hili kulishuhudiwa mapigano makali kati ya jeshi la Nchi hiyo na waasi wa M23 wanaosaidiwa na Rwanda kwenye mji wa Goma, lakini pia siasa za mataifa ya Kenya, Uganda, Tanzania na maeneo mengine duniani