Jua Haki Zako

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 3:58:48
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.

Episodios

  • Afrika Mashariki : Sikuku ya leba ina maana gani kwa wafanyakazi

    06/05/2025 Duración: 09min

    Wafanyakazi  ndio wanainua majengo, kufundisha watoto, kuwahudumia wagonjwa, kuendesha uchumi wa Afrika Mashariki. Lakini je, haki  za wafanyakazi kazini zinalindwa ? kila mwaka Mei mosi dunia huadimisha siku ya kimataifa ya wafanyakazi — na kwenye makala haya, tunaangazia kilio na matumaini ya wafanyakazi wa Afrika Mashariki wanaopigania haki zao za msingi kazini.Muungano wa kimataifa wa wafanyakazi  — ILO — linatambua haki kadhaa muhimu kwa kila mfanyakazi moja ni :Haki ya kupata mshahara wa heshimaHaki ya kufanya kazi kwa saa zinazokubalikaHaki ya kujiunga na vyamaHaki ya usalama kaziniHaki ya kutobaguliwaSkiza makala haya kufahamu mengi zaidi.

  • Tanzania: Haki ya kusikiliza kesi mahakamani

    30/04/2025 Duración: 10min

    Nchini Tanzania, wafuasi na wanasiasa wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA, walikamatwa na kupigwa na maafisa wa polisi walipokwenda Mahakamani jijini Dar es salaam, kusikiliza kesi ya uhaini na uchochezi inayomkabili kiongozi mkuu wa upinzani CHADEMA, Tundu Lissu.Katika makala ya leo ya Jua Haki yao, tunaangazia Uhuru wa kufauta kesi mahakamani, kwanini kuna haki ya kusikiliza kesi mahakamani na kwa nini mataifa mengi barani afrika yanazuia raia kusikiliza kesi kama hizi mahakamani.

  • Uchafuzi wa mazingira wakiuka haki za watoto

    24/04/2025 Duración: 09min

    Mabadiliko ya tabia nchi yametajwa kuchangia pakubwa ukiukaji wa haki za watoto. Skiza makala haya kufahamu mengi.

  • Kenya : Sanaa ya wanafunzi wa shule yakera serikali

    21/04/2025 Duración: 09min

    Mjadala makali bado unaendelea baada ya serikali kudaiwa kuzuia wanafunzi wa shule ya upili ya Butere kuwasilisha uchezo wao wa Echoas of War kwenye ngazi ya kitaifa kwenye mashindao ya kuingiza. Kisa na maana ni kwamba mchezo huo unaikosoa serikali na kwamba uliandikwa na mwanasiasa ambaye ni katibu mkuu wa zamani wa chama tawala cha UDA, Bwana Cleophas Malala. Kauli ya wanafunzi kupitia mchezo wa kuigiza wa "Echoes of Doom" imeibua maswali mazito kuhusu uhuru wa kujieleza, demokrasia na usalama wa taifa.Wanafunzi hawa walitumia jukwaa la sanaa kuelezea hali  halisi ya jamii, lakini kile kilichoanza kama onyesho la kisanaa , limeibua hisia mseto baada ya madai kwamba serikali iliwazuia wanafunzi hao kuonyesha sana hiyo kwenye ngazi ya kitaifa. Skiza makala haya kufahamu mengi zaidi.

página 2 de 2