Sinopsis
Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Episodios
-
Kenya : Haki ya mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa
17/07/2025 Duración: 09minkatika makala haya mskilizaji tunazAma kuangazia uamuzi wa kihistoria uliofanywa hivi majuzi na Mahakama ya juu zaidi ya Kenya kuhusu haki za mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa ya dini ya Kiislamu—hasa kuhusu haki ya kurithi mali ya baba yake. Uamuzi huu umetangazwa kuwa hatua muhimu katika mapambano ya kuhakikisha kila mtoto anaheshimiwa na kulindwa kikatiba bila kujali dini au mazingira ya kuzaliwa kwake. Kwa miongo mingi, baadhi ya watoto waliozaliwa nje ya ndoa, hasa katika jamii za Kiislamu, wamekuwa wakinyimwa haki ya kurithi mali ya baba zao moja kwa moja kwa mujibu tamaduni ya dini hiyo. Kufamu mengi skiza makala haya.
-
Maziwa Makuu : Haki ya afya ya akili
15/07/2025 Duración: 10minAfya ya akili ni nguzo ya kila mmoja wetu ili kuafikia haki nyingine muhimu. Benson Wakoli alifanya mazungumzo na bi Ann Maria Qwicha, mwanahabari na mtetezi wa haki za binadamu hasa afya ya akili ili kufahamu mengi zaidi katika mapambano haya ya kuhakikisha afya ya akili inalindwa.
-
Kenya : Vijana wazidi kuandamana
01/07/2025 Duración: 09minKwa wiki za hivi karibuni zimekuwa za misukosuko nchini Kenya, mitaa ya jiji la Nairobi na miji mingine mikuu imekuwa ikifurika vijana… wakiwa na mabango mikononi, miili yao ikiwa tayari kwa chochote — hata kwa gesi ya kutoa machozi na risasi. Lakini maandamano haya yanamaanisha nini? Vijana hawa wanadai nini? Na wanaruhusiwa kisheria kufanya hivyo? Ndio maswali tutakayokuwa tunayajibu kwenye makala haya. Karibu katika makala ya Jua Haki Zako – makala ambayo siku zote hukuelemisha kuhusu haki zako tena za msingi jina langu ni benson Wakoli
-
EAC : Haki za wanawake maeneo ya vita
24/06/2025 Duración: 09minKatika kila kona ya dunia, sauti za wanawake zimekuwa zikipigania jambo moja kuu – haki. Haki ya kusikilizwa, Haki ya kuthaminiwa, Haki ya kupewa nafasi sawa. Na hapa Africa Mashariki ingawa hatua zimepigwa, safari ya mwanamke kuelekea usawa bado ina changamoto, katika hali ya vita kama vile, Mashariki mwa DRC, nchini Sudan Kusini na kaskazini, kaskazini mwa Ethiopia na pia Musumbiji. Skiza makala haya kufahamu juhudi zinafanywa na shirika la Women For Women kutetea haki za wanawake kwenye maeneo ya vita, licha misaada kupunguzwa.