Sinopsis
Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa
Episodios
-
Msumbuji : Upinzani wakataa kutambua ushindi wa Daniel Chapo
05/11/2024 Duración: 10minNchini Musumbuji maandamano yamekuwa yakishuhudiwa baada ya upinzani kukataa kutambua ushindi wa mgombea wa chama tawala Daniel Chapo. Aliyekuwa mgombea wa upinzani Venancio Mondlane, amekuwa akisisitiza kwamba alipokonywa ushindi, katika makala haya tunazama kujadili kile kinachoendelea nchini Musumbiji.Wachambuzi wa siasa za kimataifa Lugete Mussa Lugete na Felix Arego wanafafanua hali nchini Msumbiji.
-
Kenya : Bunge la Kenya lamuondoa naibu rais afisini
26/10/2024 Duración: 10minNchini Kenya bunge la kitaifa na seneti limeidhinisha kuondolewa afisini kwa naibu rais Rigathi Gachagua, kutokana na tuhuma mbalimbali ikiwemo kueneza siasa za kikabila. Makala haya yaliandaliwa mapema.
-
Mgogoro kati ya rais na naibu wake nchini Kenya ambao ni mzozo wa kihistoria
23/10/2024 Duración: 10minHatma ya aliyekuwa naibu rais wa Kenya Rigathi Gachagua sasa utaamuliwa na mahakama baada ya mabunge yote mawili kumwondoa madarakani kwa njia ya hoja maalum Hatua ya kuondolewa Gachagua ni dhihirisho ya kuvunjika kwa uhusiano kati ya rais William Ruto na naibu wake Gachagua ,matukio ambayo si mageni nchini Kenya.
-
Maadhimisho ya mwaka mmoja wa shambulio la Hamas huko Gaza Oktoba 7 2024
09/10/2024 Duración: 10minMakala wimbi la siasa inaangazia maadhimisho ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kundi la Hamas, litekeleze shambulio baya zaidi kuwahi kutekelezwa huko Israeli, tukio ambalo lilianzisha vita ambayo imesababisha vifo kwa maelfu ya raia wa Kipalestina na maandamano duniani kote kupinga vita hiyo, wakati huu mzozo huo ukihofiwa kuenea katika mashariki ya kati. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka na waalikwa wake